Home Podcasts Matukio ya Taifa: Wanafunzi 42,000 kungojea zaidi kujiunga na KMTC

Matukio ya Taifa: Wanafunzi 42,000 kungojea zaidi kujiunga na KMTC

0

Zaidi ya wanafunzi elfu 42 waliokua wametuma maombi ya kujiunga na chuo cha matibabu nchini (KMTC) watalazimika kusubiri zaidi baada ya kamati ya bunge inayohusika na masuala ya afya kufutilia mbali zoezi hilo lililoendeshwa na huduma za vyuo vikuu na taasisi (KUCCPS).

Kamati hiyo ya bunge inayoongozwa na mbunge wa Endebess Dakta Robert Pukose imedai zoezi hilo liliendeshwa kinyume cha sheria baada ya mahakama kusema KUCCPS haina mamalaka kutekeleza shughuli hiyo.

kra